1. Kujaza fomu ya uanachama (TRASACCO-1b Version 2)
  2. Kulipa ada ya kiingilio TSH 50,000.00 katika benki akaunti ya chama (CRDB 0111328947801)
  3. Kulipia HISA 50 zenye thamani ya TSH 1,000,000.00 kupitia benki akaunti ya chama (CRDB 0111328947801). Unaweza kulipa HISA kwa awamu au kwa Mkupuo
  4. Tuma risiti za malipo kwa barua pepe: credit@trasaccos.co.tz
  5. Kuwasilisha fomu zilizojazwa kwa ukamilifu kwenye ofisi za Chama au kwa barua pepe info@trasaccos.co.tz
  6. Ambatanisha picha mbili za passport size.
  1. Kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika namba 6 ya mwaka 2013 Kifungu cha 41 (1) pamoja na Sera ya Mikopo, sehemu ya pili, kipengele cha 2.1.1.3 Mwanachama mpya atapata stahili ya kuomba mkopo mara baada ya kulipa kiingilio,kukamilisha angalau nusu ya Hisa za lazima na ameshaanza kukatwa michango ya akiba ya kila mwezi kutoka kwenye mshahara wake angalau kwa kipindi kisichopungua miezi miwili (2).
  2. Kipengele cha 2.1.1.4 cha Sera ya Mikopo kinaeleza kuwa Mwanachama ambaye ni mwajiriwa mpya wa Mamlaka ya Mapato atapata stahili ya kuomba mkopo baada ya kutimiza masharti ya kipengele 2.1.1.3 hapo juu na kwamba kipindi cha marejesho ya mkopo kisizidi kipindi chake cha majaribio (Probation period) ndani ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.

Mwanachama anaweza kupata taarifa zake kwa kuingia kwenye website ya TRA SACCOS (Members Portal) ataweza kuona salio la mkopo wake kwenye stetiment yake kwa kutumia nywila (password na user name) itakayomwezesha kuingia kwenye account yake.

Hivyo basi Mwanachama anatakiwa atumie Members portal ili kupata taarifa zake.

Kwa wastani malipo ya mikopo ufanyika kama ifuatavyo:

  1. Mkopo wa Papo2Papo huchukua siku 1
  2. Mkopo wa Dharura siku 3; ila kama kiasi cha mkopo hakizidi 2,000,000/=, inachukua siku 1
  3. Mkopo wa Maendeleo ya Jamii huchukua hadi siku 7
  4. Mkopo wa Elimu huchukua siku 5

NB: Ikumbukwe kwamba Mwanachama ana wajibu kuhakikisha anakamisha kujaza offer ya mkopo husika, mkataba wa mkopo pamoja na fomu mbili za wadhamini na kisha kuzirejesha ama kwa mfumo laini ama kwa kuzileta fomu halisi katika ofisi za chama kuwezesha mchakato wa kutoa mkopo huo

  1. Mkopo wa Papo2papo kiwango cha juu ni sh. 2,000,000 (Muda wa marejesho ni miezi 6).
  2. Mkopo wa Dharura kiwango cha juu ni sh. 8,000,000 muda wa marejesho ni miezi 12
  3. Mkopo wa Maendeleo ya Jamii ni mara 3 ya akiba za mwanachama ila isizidi milioni 150 (Sh150,000,000) kwa kuzingatia uwezo wa mshahara, Muda wa marejesho ni miezi 60 (Miaka 5)
  4. Mkopo wa Elimu ni mara 2 ya akiba ya elimu, Marejesho ni miezi 18
  1. Kwa mkopo wa Papo kwa Papo na Dharura mwanachama anaweza kukopa pasipo kuangalia kiasi cha akiba alichonacho kwenye Chama.
  2. Kwa mkopo wa Maendeleo ya Jamii, mwanachama atakopeshwa kiasi cha mkopo kisichozidi mara 3 ya akiba zake
  3. Kwa mkopo wa Elimu na Afya, mwanachama atakopeshwa kiasi cha mkopo kisichozidi mara 2 ya akiba zake kwenye mfuko husika.

 

18

Product Portifolio

6000+

Number of Members

3

Country Ranking

110

Billion Loan Portfolio